Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 9 Water and Irrigation Wizara ya Maji 72 2019-04-12

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Katoro- Buseresere unaokusudia kutoa maji Ziwa Victoria?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lolesia Jeremia Bukwimba, Mbunge wa Jimbo la Busanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea kutekeleza miradi ya maji ambayo lengo lake ni kufikisha huduma ya maji kwa asilimia 95 ya wakazi wa mijini na asilimia 85 ya wakazi wa vijijini hadi ifikapo mwaka 2020. Malengo hayo yanahusu pia maeneo ya Katoro na Buseresere.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza maandalizi ya utekelezaji wa mradi wa Majisafi kutoka Ziwa Victoria kwenda Miji ya Katoro na Buseresere ambapo hadi hivi sasa mazungumzo ya awali kati ya Serikali kupitia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) na wafadhili kutoka Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB) yamefanyika. EIB wameonesha nia ya kufanya mradi wa maji kwa ajili ya miji hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, andiko ya mradi wa maji kwa ajili ya miji ya Katoro na Buseresere limeshawasilishwa Wizara ya Fedha na Mipango ili maombi yaweze kuwasilishwa rasmi EIB.