Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 14 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 112 2019-04-23

Name

Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:-

Walimu wa hesabu na sayansi ni changamoto kubwa ndani ya Wilaya ya Buhigwe:-

(a) Je, ni lini Serikali itapeleka Walimu katika wilaya hiyo na waliopo sasa ni wangapi?

(b) Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa vya maabara katika shule za Buhigwe?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Albert Obama Ntabaliba, Mbunge wa Buhigwe, kama ifuatavyo.

(a) Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe ina jumla ya shule 19 zenye wanafunzi 6,622. Jumla ya Walimu waliopo wa hisabati na sayansi ni 83 sawa na asilimia 54 ya Walimu 155 wanaohitajika. Mpango wa Serikali ni kuendelea kuajiri Walimu wa masomo hayo kwa awamu na kwa sasa kibali cha kuajiri Walimu 4,549 kimekwishatolewa ambapo kati ya hao, 1,374 ni wa Masomo ya Sayansi na Hisabati. Utaratibu wa kuajiri Walimu hao unaendelea na watapangwa kwenye halmashauri zenye upungufu mkubwa ikiwemo Halmashauri ya Buhigwe.

(b) Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2017/ 2018, Halmashauri ya Buhigwe ilipokea vifaa vya maabara kwa shule mbili za sekondari zilizokamilisha ujenzi wa maabara. Vilevile katika Mwaka 2018/2019 Serikali inatarajia kununua na kusambaza vifaa vya maabara kwenye shule za sekondari 1,250 zikiwemo shule za sekondari katika Halmashauri ya Buhigwe zilizokamilisha vyumba vya maabara.