Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 19 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 154 2019-05-02

Name

Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE (K.n.y. MHE. SELEMANI S. BUNGARA) aliuliza:-

Hospitali ya Wilaya ya Kilwa haina Jokofu la kuhifadhi maiti na pia majengo yake mengi ni chakavu:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kununua jokofu jipya sambamba na kukarabati majengo ya hospitali hiyo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE.MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Selemani Saidi Bungara, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti Hospitali ya Wilaya ya Kilwa (Kinyonga)ni miongoni mwa Hospitali Kongwe za Wilaya hapa nchini na imekuwepo tangu mwaka 1965. Kwa kutambua umuhimu wa Hospitali hiyo, Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo imekua ikifanya ukarabati na upanuzi wa majengo mbalimbali ya kutolea huduma kama ifuatavyo:-

Mwaka wa Fedha 1996/1997, ukarabati wa miundombinu mbalimbali ya hospitali ulifanyika pamoja na ujenzi wa kliniki ya Mama na Mtoto; Mwaka 2010 ulifanyika ujenzi wa Jengo la Huduma za UKIMWI (CTC); Mwaka 2012 ulifanyika ujenzi wa jengo la wazazi; na Mwaka 2017 ulifanyika ujenzi wa jengo la mama ngojea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Wilaya ya Kilwa ina jokofu moja la kuhifadhia maiti lililonunuliwa mwaka 1996. Hata hivyo, jokofu hilo lina uwezo wa kuhifadhi mwili mmoja tu. Serikali inaendelea nautaratibu wa kukamilisha hatua za kuanza ujenzi wa jengo jipya la kuhifadhia maiti kwenye hospitali hiyo sambamba na ununuzi wa jokofu jipya la kisasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kukarabati miundombinu ya vituo vya kutolea huduma za afya nchini kwa kadri ya upatikanaji wa rasilimali fedha utakavyokuwa.