Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 21 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 166 2019-05-06

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:-

Mtambo wa kuchoma takataka za hospitali na dawa zilizokwisha muda wake upo katika Kijiji cha Dundani Wilayani Mkuranga. Uchomaji unapofanyika moshi mzito huingia kwenye nyumba na maeneo ya wananchi wanaoishi karibu na mtambo huo na kuhatarisha afya zao:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kunusuru afya na maisha ya wananchi wanaoishi karibu na mtambo huo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ruth Hiyob Mollel, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba upo mtambo wa kuchomea taka na dawa zilizokwisha muda wake uliojengwa na mwekezaji katika Kijiji cha Dundani, Wilaya ya Mkuranga. Hapo awali mtambo huo ulikuwa na kasoro za ujenzi ambapo Serikali ilimwagiza mwekezaji kuzirekebisha kwa ilani ya tarehe 18, Oktoba, 2017 yenye kumbu. Na. NEMC/HQ/EA/05/0702/VOL1/7 sambamba na kusimamisha shughuli za mtambo mpaka kasoro zitakapokuwa zimerekebishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, marekebisho hayo yamefanyika na baada ya mamlaka zote, ikiwemo Serikali ya Kijiji cha Dundani kujiridhisha kwamba hakuna tena moshi unaoathiri mazingira, mtambo huo umeruhusiwa kuendelea na kazi na mpaka sasa hakuna taarifa yoyote iliyofika katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, Wilaya ya Mkuranga kulalamikia shughuli za mtambo huo.