Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 27 2020-01-30

Name

Andrew John Chenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Primary Question

MHE. ANDREW J. CHENGE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha ahadi yake ya kujenga barabara za Mji wa Bariadi kwa Kiwango cha lami?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Andrew John Chenge, Mbunge wa Bariadi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza ahadi yake ya ujenzi wa barabara katika Mji wa Bariadi kwa kiwango cha lami kwa kujenga barabara zenye urefuwa kilometa 7.76 kwa kiwango cha lami, njia za waenda kwa miguu kilometa 9.4, mitaro ya maji ya mvua yenye urefu wa kilometa 10.11 na uwekaji wa taa 302 chini ya mradi wa uendelezaji miundombinu katika miji (Urban Local Governments Strengthening Project-ULGSP).

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kujenga na kukarabati miundombinu ya barabara na madaraja katika Mji wa Bariadi kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Ahsante.