Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 3 Water and Irrigation Wizara ya Maji 36 2020-01-30

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:-

Serikali inatekeleza mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria na kuyapeleka Mkoa wa Tabora katika Miji ya Igunga, Nzega, Manispaa ya Tabora, Sikonge, Isikizya na Urambo:-

(a) Je, ni vijiji gani vya Mashariki vya Jimbo la Tabora Kaskazini – Uyui vitapatiwa maji kutokana na mradi huo?

(b) Kwa vile ni idadi ndogo tu ya vijiji kati ya 82 vya Jimbo la Tabora Kaskazini ndiyo vitapatiwa maji na mradi huo: Je, Serikali ina mpango gani wa kuvipata maji vijiji vyote katika Jimbo la Tabora Kaskazini?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kwenye Miji ya Tabora, Igunga na Nzega pamoja na vijiji zaidi ya 102 vilivyopo umbali wa kilomita 12 kila upande kutoka bomba kuu. Vijiji vilivyopo Jimbo la Tabora Kaskazini katika mradi huu ni 26 ambavyo ni Igoko, Isikizya, Ikonolo, Mswa, Itobola, Isenegenzya, Majengo, Ikongolo, Kanyenye, Kiwembe na Kalemela,

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Serikali imeanza kutekeleza miradi katika miji 28 kupitia mkopo wa Dola za Marekani milioni 500 kutoka Benki ya Exim ya India. Mradi huo utapeleka maji katika Miji ya Sikonge, Urambo, Kaliua na baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Uyui kwa kutoa maji Ziwa Victoria. Mpaka sasa vijiji vilivyotambuliwa wakati wa usanifu wa kupeleka maji Sikonge, Urambo na Kaliua ni 14 ambavyo ni Kasisi B, Ilalongulu, Mpenge, Isenga, Ngokolo, Ulimakafu, Mabama, Tumaini, Maswanya, Chali Ndono, Itinka, Tulieni na Utemini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, kwa miradi yote miwili itahudumia jumla ya vijiji 40 vya Jimbo la Tabora Kaskazini. Serikali itaendelea kutenga na kutoa fedha ili kuhakikisha vijiji vyote vilivyobaki vinapata huduma ya maji.