Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 66 2020-02-04

Name

Amina Nassoro Makilagi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA N. MAKILAGI aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha miundombinu ya Kituo cha Afya cha Kiagata kwani Wananchi wote wa Wilaya ya Butiama wanategemea Kituo hicho?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA Z A MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Nassor Makilagi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyeiti, katika mwaka wa fedha 2017/2028 Serikali iliidhinisha na kutoa kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya kuboresha miundmbinu ya Kituo cha Afya cha Kiagati. Kazi zilizofanyika ni ujenzi wa nyumba ya mtumishi, wodi ya wazazi, jengo la maabara, jengo la mionzi, jengo la kuhifadhia maiti na kichomea taka. Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kupitia mapato yake ya ndani imetumia kiasi cha shilingi milioni 37.5 kwaajili ya kukamilisha miundombinu iliyosalia pamnoja na kununua Jokofu la kuhifadhia maiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, KItuo hicho cha afya kwa sasa kinatoa huduma za upasuaji wa dharura, huduma za ultrasound, huduma za Mama na Mtoto na kulaza wagonjwa.