Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 74 2020-02-04

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-

Je, Serikali inahakikishaje amani na utulivu vinakuwepo katika chaguzi mbalimbali nchini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maftaha Abdallah Nachuma Mbunge wa Mtwara Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwafahamisha wananchi kuwa ni jukumu la Serikali kuhakikisha kuwa amani na utulivu vinatamalaki nchini wakati wote bila kujali nyakati au majira mbalimbali katika mwaka. Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama limejipanga vizuri kudhibiti vitendo mbalimbali vya uvunjaji wa sheria ikiwemo fujo au aina yeyote ya ukosefu wa amani vinavyoweza kusababisha wananchi kushindwa kushiriki katika shughuli zao za kila siku, ikiwemo kushiriki katika michakato ya chaguzi mbalimbali zinazofanyika nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Polisi inaendelea kutoa mafunzo mbalimbali kwa askari wake wa ukakamavu, upelelezi na kuongeza vifaa vya kutenda kazi ili kuwajengea uwezo na weledi mkubwa wa kuweza kuzuia na kukabiliana na vitendo kama hivyo vinavyojitokeza nyakati za uchaguzi.