Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 3 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 35 2019-09-05

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:-

Kambi za Jeshi 41KJ, 452 Medium ni miongoni mwa kambi kongwe na zenye mchango mkubwa katika Ulinzi wa Taifa letu. Kutokana na ukongwe huo, kambi hizo zimechakaa miundombinu yake mfano shule na zahanati zilizopo kwenye kambi hizo:-

(a) Je, nini mpango wa Serikali juu ya kuboresha miundombinu ya Zahanati zilizopo kwenye kambi hizi?

(b) Je, nini mpango wa Serikali wa kuboresha miundombinu ya shule hiyo iliyopo kwenye kambi hizo?

(c) Je, nini mpango wa Serikali juu ya kuboresha miundombinu ya Medium Workshop hiyo?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Elias Masala, Mbunge wa Nachingwea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi ya Jeshi 41KJ na 451KJ ni miongoni mwa kambi kongwe na zenye mchango mkubwa katika ulizi wa Taifa letu. Kutokana na ukongwe wa kambi hizo, umepelekea kuchakaa kwa miundombinu ya zahanati, shule na medium workshops zilizopo huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uboreshwaji wa miundombinu ya hospitali kuu ya kanda iliyopo chini ya kambi ya Jeshi la 41 KJ, umekamilika likiwemo jengo kuu la hospitali, wodi za wagonjwa, chumba cha kuhifadhia maiti pamoja na vitanda vya malazi na kujifungulia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto iliyopo ni upungufu wa wataalam pamoja na madawa, ambapo kwa hatua za awali Jeshi la Wananchi wa Tanzania tayari limeshawaandikisha madaktari 300 ambao wamepelekwa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli na wanatarajiwa kutawanywa katika hospitali na vituo vya afya mbalimbali nchini, ikiwemo hospitali kuu ya kanda iliyopo 41KJ. Changamoto ya upungufu wa madawa itashughulikiwa kadri ya fedha zinatakavyopatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, 451KJ, ina kituo kidogo cha afya ambacho hutoa huduma ya kwanza kwa Maafisa, Askari, pamoja na raia waliopo jirani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule inayozungumziwa hapa ni Shule ya Msingi ya Maji Maji iliyopo katika Kambi ya Jeshi 41KJ. Kwa nyakati tofauti Serikali imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu mbalimbali ya shule za msingi zikiwemo shule zilizopo katika maeneo ya Jeshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara inaendelea kufanya mawasiliano na Wizara yenye dhamana ya kusimamia Shule za Msingi (TAMISEMI) ili ione uwezekano wa kutenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya Shule ya Msingi Maji Maji iliyopo katika Kambi ya Jeshi 41KJ Wilayani Nachingwea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha za bajeti zimekuwa hazitosherezi katika kufufua karakara hiyo, hivyo Jeshi la Wananchi Tanzania limeweka mikakati ya kufufua miundombinu ya karakana ili iweze kujiendesha kibiashara kwa ajili ya kulihudumia Jeshi na Wananchi kwa ujumla. Aidha, mchakato wa kuipeleka karakana hiyo katika ngazi ya VETA unaendelea chini ya Makao Makuu ya Jeshi.