Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 44 2019-09-06

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOYCE B. SOKOMBI (K.n.y. MHE. ESTHER N. MATIKO) aliuliza:-

Serikali imekuwa ikitoa vifaa tiba na dawa vyenye thamani ya Tsh. 4,000,000/= kila baada ya miezi mitatu kwenye zahanati za Halmashauri za Mji wa Tarime kupitia Wakala wa dawa (MSD); kwa miaka miwili iliyopita Serikali imepunguza ugawaji wa dawa na vifaa tiba kutoka thamani ya Tsh. 4,000,000/= mpaka Tsh. 166,000/=; mfano zahanati ya Gamasara imepokea dawa na vifaa tiba vyenye thamani hiyo:-

Je, ni kwa nini Serikali iliamua kupunguza mgao wa dawa kutoka Tsh. 4,000,000/= mpaka Tsh. 166,000/= ilhali idadi ya watu inazidi kuongezeka katika Halmashauri ya Mji wa Tarime na Majimbo ya jirani?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini, kama Ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupungua kwa bajeti ya dawa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime kunatokana na tathmini ya uwezo wa kuagiza na kutumia dawa wa vituo vya kutolea dawa katika Mji wa Tarime. Mfano, Zahanati ya Gamasara, ilitengewa na kupatiwa kiasi cha shilingi milioni
17.25 katika mwaka wa fedha 2018/2019 na tarehe 30 Juni, 2019, zahanati hiyo ilikuwa imetumia kiasi cha shilingi milioni
4.25 pekee na hivyo kiasi cha shilingi milioni 13 ilichopewa kutumia katika mwaka husika kubakia Bohari ya Dawa (MSD). Hivyo tunazielekeza Halmashauri zote na vituo vya kutolea huduma za afya, kwamba wawe wanazingatia mipango yao ya bajeti katika manunuzi ya dawa na vifaa tiba ili kuweza kuhudumia wananchi ipasavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.