Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 82 2020-02-05

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU aliuliza:-

Kazi zote za Utawala na fedha katika Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali za Wilaya zinasimamiwa na Mganga Mfawidhi wa Wilaya wa eneo husika:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapa elimu ya Utawala na Usimamizi wa Fedha Madaktari hao ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zaynabu Matitu Vulu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali iliajiri Wahasibu Wasaidizi 335 na kuwapanga kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili kuimarisha usimamizi wa fedha kwenye Vituo vya Afya kupitia mfumo wa kielektroniki wa Facility Financing, Accounting and Reporting System (FARS). Aidha, ili kukabiliana na upungufu uliopo wa wataalam hao wa utawala na usimamizi wa fedha, Waganga Wafawidhi katika Hospitali za Halmashauri, Vituo vya
Afya na Zahanati wamepatiwa mafunzo ya utawala na usimamizi wa fedha yaliyofanyika kuanzia tarehe 24 Desemba, 2018 hadi tarehe 22 Januari, 2019 katika kila Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, lengo la mafunzo hayo lilikuwa ni kuwajengea uwezo wataalam hao kwenye masuala ya fedha na utawala katika vituo wanavyovisimamia. Ofisi ya Rais, TAMISEMI imewasilisha maombi ya kibali cha kuajiri zaidi watumishi wa kada za Wahasibu Wasaidizi kwa lengo la kuimarisha utawala na usimamizi wa fedha kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.