Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 91 2020-02-05

Name

Dua William Nkurua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. WILLIAM D. NKURUA aliuliza:-

Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Nanyumbu kinatumia majengo ya nyumba za kuishi Askari Polisi:-

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Nanyumbu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa William Dua Nkurua, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Nanyumbu ni miongoni mwa wilaya mpya ambayo ilianzishwa mwaka 2007 hivyo baada ya mabadiliko haya ililazimu jengo ambalo lilikuwa likitumika kama Kituo kidogo cha Polisi kata kuanza kutumika kama Kituo cha Polisi Wilaya.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi inatambua changamoto za ukosefu wa vituo vya polisi na ofisi katika wilaya mpya zilizoanzishwa hivi karibuni ikiwemo Wilaya ya Nanyumbu. Jitihada zinaendelea kufanyika za ujenzi wa vituo vya polisi na ofisi za wakuu wa polisi wa wilaya hizo kadiri fedha kutoka kwenye bajeti ya maendeleo na vyanzo vingine vinavyopatikana.