Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 95 2020-02-05

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha miradi ya umeme Vijijini katika vijiji ambavyo bado havijafikiwa Wilayani Chunya?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa, Mbunge wa Lupa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi kabambe wa kusambaza umeme vijijini ambapo kwa sasa unatekelezwa kupitia Awamu ya III Mzunguko wa Kwanza unaoendelea utakaokamilika mwezi Juni, 2020.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Chunya ina vijiji 43, kati ya vijiji hivyo, vijiji 37 tayari vimeshapatiwa umeme vikiwemo Vijiji vya Chokaa, Ifumbo, Isewe, Kibaoni, Lola, Kiwanja, Mlimanjiwa pamoja na Lupatingatinga. Utekelezaji wa kazi hii umekamilishwa na Mkandarasi STEG International Services na uligharimu shilingi bilioni 4.2.

Mheshimiwa Spika, vijiji vilivyobaki katika Wilaya ya Chunya vitapelekewa umeme kupitia Mradi wa REA Mzunguko wa Pili pamoja na miradi mingine ya densification kwa maana ya ujazilizi, itakayoanza mwezi Februari, mwaka huu 2020 na kukamilika ifikapo mwezi Juni, mwaka 2021.