Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 97 2020-02-06

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. WILLY Q. QAMBALO aliuliza:-

Mabaraza ya Ardhi ya Kata ni chombo muhimu sana katika kutatua migogoro ya ardhi. Hata hivyo, changamoto kubwa ni uwezeshaji (chakula na nauli) na wajumbe wa mabaraza hayo ili wafanye kazi zao kwa weledi. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wajumbe wanawezeshwa ili waweze kutoa haki?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Qambalo Willy Qulwi, Mbunge wa Karatu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kifungu cha 7 cha Sheria ya Mabaraza ya Ardhi ya Kata kinazipa Halmashauri wajibu wa kutengeneza utaratibu wa namna ya kuwezesha Mabaraza ya Ardhi na Kata kiutendaji na kuweka mazingira mazuri ya kufanyia kazi. Mikoa na Wilaya imeelekezwa kuzisimamia Halmashauri kuhakikisha Mabaraza hayo yanawezeshwa ili yaweze kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu. Kila Halmashauri inatakiwa kutenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya kuhudumia Mabaraza ya Ardhi ya Kata. Ofisi ya Rais, TAMISEMI inaendelea kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji ili kuhakikisha changamoto hiyo inapatiwa ufumbuzi, ahsante.