Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 78 2019-11-12

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:-

Wilaya ya Uvinza imeanzishwa tangu mwaka 2002 lakini hadi sasa Jeshi la Polisi katika Wilaya hii halina nyumba za kuishi, Ofisi pamoja na vitendea kazi:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vitendea kazi Jeshi la Polisi katika Wilaya hiyo kama vile magari, Ofisi pamoja na makazi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hasna Sudi Mwilima, Mbunge Wa Kigoma Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Polisi lina jumla ya Wilaya 168 za kipolisi ikiwa ni pamoja na Wilaya za Kiserikali. Kati ya hizo Wilaya 127 zina majengo kwa ajili ya Ofisi na Vituo vya Polisi vya Wilaya ikiwemo Wilaya ya Uvinza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kufanya jitihada mbalimbali kuliboresha Jeshi la Polisi kwa awamu. Mathalani, Serikali imejenga na inaendelea kujenga nyumba za makazi kwa askari nchi nzima katika ngazi ya Mkoa na ni mpango wa Serikali kujenga Ofisi na nyumba za kuishi askari katika ngazi za wilaya zote nchini. Aidha, Wilaya ya Uvinza ina magari mawili ambayo ni T/Land cruiser PT 1415 linalotumiwa na OCD na Leyland Ashock kwa matumizi mbalimbali ya Kipolisi.