Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 6 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 75 2019-09-10

Name

Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS NYIMBO Aliuliza:-

Je, Serikali ina maelezo gani juu ya viongozi kutoka nje ya nchi wanaokuja Tanzania na kutembelea baadhi ya maeneo na kisha wanapokuta miradi ya wananchi huahidi kusaidia na baadae kushindwa kutimiza ahadi zao?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI Alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tauhida Cassian Gallos, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania imekuwa ikipokea viongozi wageni kutoka nje ya nchi na makundi aina mbili yaani wa Kiserikali na wasio wa Kiserikali. Viongozi hao hutembelea Tanzania kwa ziara za kikazi na binafsi ambapo hupata fursa ya kuona miradi ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ina jukumu la kuratibu na kusimamia ziara za kikazi za viongozi wa Serikali kutoka mataifa ya kigeni ikiwa ni pamoja na kufuatilia utekelezaji wa ahadi mbalimbali zinazotolewa na viongozi hao kwa kushirikiana na Wizara za kisekta na taasisi za Kiserikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ambazo hutolewa na baadaye kushindwa kutimizwa, Wizara huratibu vikao vya majadiliano vinavyoshirikisha wahusika pamoja na Wizara za kisekta na taasisi za Kiserikali ili kupata mwafaka juu ya suala husika.