Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 82 2019-09-10

Name

Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA (K.n.y. MHE. PETER A. LIJUALIKALI) Aliuliza:-

Jeshi la Magereza lilikuwa na mpango wa ujenzi wa Gereza Kitongoji cha Nakato na Kijiji cha Kibaoni, Wilaya ya Kilombero.

Je, mpango huu umefikia wapi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI Alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Peter Ambrose Lijualikali, Mbunge wa Kilombero kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kilombero ni miongoni mwa Wilaya 51 nchini ambazo hazina magereza. Mpango wa kuwa na magereza katika kila Wilaya una lengo la kupunguza tatizo la msongamano kwenye baadhi ya magereza yanayopokea wahalifu kutoka Wilaya zisizokuwa na magereza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa kuwa na magereza kila Wilaya utarahisisha usikilizwaji wa kesi, wafungwa na mahabusu wataweza kupata huduma kwa urahisi kutoka kwa mawakili wao na pia kupunguza gharama za usafiri kwa ndugu zao wanapowatembelea magerezani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Magareza ina mpango wa kujenga magereza kwa Wilaya ambazo hazina magereza nchini ikiwemo Wilaya ya Kilombero. Aidha, mpango huu utatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha.