Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 28 2016-01-27

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. JAMES F. MBATIA (K.n.y. MHE. JOHN J. MNYIKA) aliuliza:-
Pamoja na kuwa karibu na Makao Makuu ya TANESCO, baadhi ya maeneo ya Jimbo la Kibamba hayana umeme na yale yenye umeme kiwango chake hupungua na kuongezeka (low voltage and fluctuation):-
(a) Je, Serikali inaweza kuwasilisha orodha ya maeneo yasiyo na umeme katika Kata za Saranga, Mbezi, Msigani, Goba , Kwembe na Kibamba, na lini maeneo hayo yatapatiwa umeme; (TANESCO)?
(b) Je, Serikali ina inachukua hatua gani kuondoa tatizo la kupungua na kuongezeka kwa umeme katika Kata hizo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa John John Mnyika, Mbunge wa Kibamba, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, orodha ya maeneo yasiyo na umeme katika Kata ya Saranga, Mbezi, Msigani, Goba, Kwembe pamoja na Kibamba ni kama yafuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Kata ya Saranga ni Saranga Ukombozi na Nzasa na yanatarajiwa kupatiwa umeme mwezi Mei mwaka huu; Kata ya Msigani na Marambamawili inatarajiwa pia kupata huduma za umeme mwezi Aprili, mwaka huu; Kata ya Goba na Kata ya Goba Mpakani inatarajiwa pia kupata umeme mwezi Septemba, mwaka huu; Kata ya Kwemba ni King‟azi „B‟ itakayopatiwa umeme mwezi Septemba, mwaka huu; na Kisokwa ambalo limeombewa fedha kwenye bajeti ya TANESCO mwaka 2016/2017.
Pia Kata ya Mbezi ni Kibesa inayoombewa fedha katika bajeti ya TANESCO ya mwaka 2016/2017; na Msumi ambalo inapatiwa umeme mwezi Mei, mwaka huu; na katika Kata ya Kibamba maeneo yote yamefikiwa na umeme wa huduma iliyopita.
Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na tatizo la kupungua na kuongezeka kwa umeme katika Kata hizo, ukarabati wa miundombinu unatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia mwezi Februari, 2016 na pia unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2016.
Kazi zitakazohusishwa na ukarabari huo ni pamoja na kuongeza njia ya umeme toka njia moja hadi njia tatu, yaani (upgrading), lakini kufunga nyaya zenye uwezo mkubwa wa kuondoa tatizo la kupungua kwa umeme chini ya utaratibu unaoitwa re-conductoring. Aidha, kutakuwa na ufungaji wa transfoma kubwa na kuondoa ndogo ili kukidhi mahitaji ya umeme katika maeneo husika.