Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 17 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 146 2016-05-11

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Makazi ya askari yamekuwa ya zamani pia mengine yamekuwa mabovu sana, mfano nyumba za Ziwani Zanzibar, Wete, Pemba na Chakechake Pemba hazikaliki kabisa.
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifanyia marekebisho nyumba hizo?
(b) Je, ni gharama gani Serikali itatumia kwa marekebisho ya nyumba hizo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mattar Ali Salum, Mbunge wa Shaurimoyo lenye sehemu (a), na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nyumba nyingi za makazi ya askari hazijafanyiwa ukarabati zikiwemo za Ziwani Zanzibar, Wete na Chakechake. Serikali ina mpango wa kuzifanyia marekebisho nyumba zote za polisi Unguja na Pemba kwa kadri uwezo wa fedha utakavyoongezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, gharama halisi za ukarabati wa nyumba zote za polisi Unguja na Pemba ni bilioni 1.5.