Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 17 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 147 2016-05-11

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:-
Wananchi wa Kijiji cha Busiri, Wilayani Biharamulo ni miongoni mwa Watanzania wanaoendesha maisha yao kwa shughuli za uchimbaji mdogo mdogo ambazo zinahitaji kuungwa mkono na Serikali kimkakati.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaunga mkono wachimbaji wadogo wadogo wa Busiri?
Je, Serikali iko tayari kuwatembelea wananchi wa Busiri na kuwaelewesha ni namna gani na ni lini itaanza kutekeleza mkakati huo wa kuwaunga mkono wachimbaji wadogo wadogo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oscar Rwegasira Mukasa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya mikakati ambayo Serikali imechukua kwa wachimbaji wadogo wa madini hasa katika eneo la Busiri ni kuwatafutia maeneo ya uchimbaji wa madini. Wizara imetenga eneo lenye ukubwa wa takribani hekta 11,031 lililoko chini ya leseni za utafutaji wa madini namba 3220 ya mwaka 2005 iliyokuwa inamilikiwa na Ndugu Daudi Mbaga. Kadhalika katika eneo hilo la leseni ya utafutaji wa madini namba 5853 ya mwaka 2009 iliyokuwa chini ya kampuni Meru Resource Limited ambazo zote zimemaliza muda wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi mwisho wa mwezi Machi mwaka jana na mwisho wa mwezi Machi mwaka huu Wizara imegawa kwa wananchi wa Busiri leseni 81 zenye uchimbaji mdogo wa madini ambazo kwa ujumla wake zinachukua hekta 810 kati ya hekta 11,031 za eneo hilo. Aidha, Wizara imegawa leseni nyingine 30 za uchimbaji mdogo katika eneo lililoko katika karibu na eneo hilo takribani kilometa moja tu kutoka eneo la uchimbaji mdogo wa madini la Busiri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati mwingine ni kuendelea kulitumia eneo la Shirika la STAMICO kutoa huduma za ugani kwa wachimbaji madini wadogo hasa wa kijiji cha Busiri na maeneo mengine nchini. Mkakati mwingine ni kuwapatia ruzuku pamoja na kuwapatia elimu endelevu itakayoendelea kutolewa pamoja na shirika la STAMICO.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikiwatembelea wachimbaji hawa mara kwa mara hasa kwa kutumia Maafisa na wataalam wa ofisi ya Kanda ya Ziwa Victoria Magharibi na Afisi Madini Mkazi wa ofisi ya Bukoba. Tarehe 11 Machi, 2016 Afisa Madini Mkazi wa Bukoba alifika na kufanya mkutano na kikundi cha Busiri Mining Co-operative Society Limited chenye leseni ya uchimbaji mdogo. Aidha, ili kutekeleza sasa ombi la Mheshimiwa Mbunge Wizara yangu itamtuma tena Afisa Madini kutembelea eneo hilo na kuwaelimisha wananchi juu ya uchimbaji mzuri mdogo wa madini katika eneo hilo.