Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 17 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 148 2016-05-11

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. COSTANTINE J. KANYASU (K.n.y MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA) aliuliza:-
Mkandarasi wa REA anayefunga umeme katika Jimbo la Geita Vijijini amemaliza tatizo na yule anayeunganisha kutoka Sengerema yupo pole pole sana.
Je, ni lini sasa Serikali itamsimamia kikamilifu mkandarasi huyo ili aweze kumaliza kazi hiyo na umeme uweze kuwashwa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Musukuma Joseph Kasheku, Mbunge wa Geita Vijijini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa REA Awamu ya II katika Mkoa wa Geita likiwemo Jimbo la Geita Vijijini unatekelezwa na mkandarasi Nakuroi Investiment Company Limited. Kazi ya kupeleka umeme Geita inajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 161.5; ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 119.2; ufungaji wa transfoma 49 za ukubwa mbalimbali. Pamoja na hayo pia kuunganisha umeme wateja wa awali 2,560 na kazi za mradi zimekamilika kwa asilimia 94 ambapo ujenzi wa laini kubwa umekamilika kwa asilimia 100 na ujenzi wa laini ndogo umekamilika kwa asilimia 84. Kadhalika ufungaji wa transfoma 29 zimefungwa na wateja 846 wameunganishiwa umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, umeme umeshafika Nyamadoke kutoka Sengerema Mkandarasi ameelekezwa sasa kuhakikisha kwamba, kazi zote za kuunganisha zinakamilika ifikapo mwezi June mwaka huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, REA pamoja na TANESCO wameongeza kasi sasa ya kumsimamia Mkandarasi huyu ili kuhakikisha kwamba kazi za ujenzi zinakamilika ifikapo Juni mwaka huu.