Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 24 Water and Irrigation Wizara ya Maji 204 2021-05-06

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga miundombinu ya maji katika vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Elibariki Immanuel Kingu, Mbunge wa Singida Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto ya hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Jimbo la Singida Magharibi. Ili kuendelea kutatua changamoto hiyo, Serikali imekamilisha upatikanaji wa vyanzo vya maji kwa kuchimba visima virefu katika Vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, uendelezaji wa visima hivyo kwa kujenga miundombinu ya usambazaji utaanza mwaka wa fedha 2021/2022 ambapo kazi zitakazofanyika ni pamoja ununuzi na ufungaji wa pampu saba, ujenzi wa nyumba za mashine saba, matanki ya kuhifadhi maji saba yenye ukubwa lita 90,000 na 100,000 na ununuzi na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji umbali wa kilometa 85.9 na ujenzi wa vituo vya kuchotea maji 79. Pia, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 imepanga kutekeleza miradi minne ya ujenzi wa miundombinu ya maji katika vijiji vya Irisya, Iglansoni, Ihanja na Kaugeri vilivyopo katika Jimbo Singida Magharibi. (Makofi)