Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 51 Enviroment Ofisi ya Rais TAMISEMI. 434 2016-06-27

Name

Hassan Selemani Kaunje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. KAUNJE aliuliza:-
Jimbo la Lindi Mjini lina eneo la Bahari ya Hindi lenye urefu wa kilometa 112, lakini eneo hilo halina mchango wowote wa maana kwenye pato la Taifa na Manispaa ya Lindi:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza eneo la bahari katika Manispaa ya Lindi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Kaunje, Mbunge wa Lindi Mjini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuendeleza eneo la ukanda wa bahari ya Hindi katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, Serikali imeendelea na maandalizi ya mpango wa upimaji wa muda mrefu yaani master plan wa wilaya nzima ambao utaainisha matumizi mbalimbali ya ardhi, yakiwemo uwekezaji, makazi na matumizi mengine. Tayari kibali cha kuandaa mpango huo kimeshatolewa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Halmashauri. Kwa sasa mkataba wa kazi hiyo, uko kwa Mwanasheria Mkuu kwa ajili ya uhakiki yaani vetting ili taratibu za kupata mzabuni ziendelee.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango huo utahusisha uboreshaji wa makazi holela yaani resettlement scheme katika eneo la Mnazi Mingoyo, Mpilipili na Rahaleo ili kuwa na mji wa kisasa katika Manispaa ya Lindi. Kazi zote hizo zinatarajiwa kugharimu jumla ya shilingi bilioni moja hadi kukamilika kwake. Mpango huo utakapokamilika utasaidia Serikali kupata mapato kutokana na aina ya uwekezaji utakaofanyika katika ukanda huo wa bahari ndani ya Manispaa ya Lindi.