Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 42 2022-02-07

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. ERIC J. SHIGONGO Aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itarejesha Mamlaka kwa Madiwani ya kuzisimamia halmashauri zao pamoja na kuwaazimia Wakurugenzi wa Halmashauri pale linapotokea tatizo kwenye halmashauri husika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Eric James Shigongo, Mbunge wa Jimbo la Buchosa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mamlaka za ajira na nidhamu kwa Watumishi wa Halmashauri hutofautiana kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Namba 8 ya mwaka 2002 na Kanuni zake za mwaka 2003. Kwa mujibu wa Sheria hii Mamlaka ya nidhamu ya Wakurugenzi wa Halmashauri za Majiji ni Katibu Mkuu Kiongozi na Mamlaka ya nidhamu ya Wakurugenzi wa Halmashauri za Manispaa, Miji na Wilaya ni Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Spika, halmashauri kupitia Baraza la Madiwani imepewa Mamlaka ya kusimamia nidhamu ya watumishi wengine wote wa halmashauri wakiwemo Wakuu wa Idara kwa kuzingatia kifungu cha 6 (6) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Namba 8 ya mwaka 2002 na Kanuni zake za Mwaka 2003.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia Sheria hizo Waheshimiwa Madiwani hawana Mamlaka ya kuwawajibisha Wakurugenzi, ikitokea tatizo katika utendaji wa Mkurugenzi wa Halmashauri wanapaswa kutoa taarifa kwa Mamlaka husika. Ahsante.