Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 39 2016-01-29

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:-
Mkoa wa Katavi ni moja kati ya mikoa iliyoanzishwa hivi karibuni ili kusogeza karibu na wananchi huduma muhimu za Serikali lakini mkoa huo hauna Hospitali ya Mkoa na Serikali ilishaamua kujenga hospitali hiyo na Serikali ya Mkoa ilishatenga eneo kwa ajili ya ujenzi.
(a) Je, ni lini utekelezaji wa mradi huo utaanza?
(b) Jiografia ya Mkoa wa Katavi ni pembezoni mwa nchi; je, hiyo inaweza kuwa sababu ya kusuasua kwa mradi huo na kupita takribani miaka minne sasa toka Serikali ifanye uamuzi huo lakini hakuna hata dalili chanya kuelekea kukamilika kwa mradi huo?

Name

Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimia Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Mpanda Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, maandalizi ya ujenzi ya Hospitali ya Mkoa wa Katavi yanaendelea ambapo tayari eneo lenye ukubwa wa ekari 243 limepatikana na fidia ya shilingi milioni 468 imeshalipwa kwa wananchi waliopisha maeneo yao kuruhusu ujenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka 2015/2016, Mkoa umetenga shilingi bilioni moja ambazo zitatumika kuandaa michoro na kuanza ujenzi. Mkoa unasubiri kibali cha Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili Mshauri Mwelekezi aweze kuanza kuandaa michoro yaani master plan na kuendelea na hatua nyingine za ujenzi.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali ni kuwa na Hospitali ya Rufaa kwa kila mkoa. Hivyo, Mkoa wa Katavi ni miongoni mwa mikoa mipya itakayojengwa Hospitali ya Mkoa ili kusogeza huduma za afya kwa ajili ya wananchi.