Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 139 2022-09-23

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kupitia upya mfumo wa haki jinai ili kupunguza changamoto ya idadi kubwa ya mahabusu kuliko wafungwa magerezani?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria naomba kumjibu Mheshimiwa Neema Kichiki Lugangira, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuhakikisha maboresho ya mfumo wa haki jinai nchini yanafanyika ili kuimarisha upatikanaji wa haki jinai nchini ikiwemo kuondokana na mlundikano wa mahabusu katika magereza yetu. Kutokana na umuhimu huo, Wizara imeandaa andiko la mapendekezo ya maboresho ya mfumo wa haki jinai ikishirikiana na Taasisi Zisizo za Kiserikali, Taasisi za Dini na Vyuo vinavyotoa elimu ya sheria ili kuhakikisha kwamba Mfumo wa Haki Jinai unafanyiwa marekebisho na kuwekwa sawa. Ahsante.

SPIKA: Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali nakuona umesimama.

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu yaliyotolewa na Mheshimiwa Naibu wa Waziri wa Ardhi kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria ningependa kurejesha kumbukumbu sahihi za kazi ya Bunge hili kwamba Sheria Namba 1 ya mwaka 2022 iliyotungwa na Bunge hili mwezi wa pili ilizuia kufikishwa mahakamani kwa kesi ambazo upelelezi bado isipokuwa kwa makosa yale makubwa. Hiyo ni hatua moja kubwa sana na iliyolenga kupunguza msongamano wa mahabusu. (Makofi)