Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 20 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 172 2016-05-16

Name

Godfrey William Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

Kuwawezesha Wananchi Kupata Umeme wa Bei Nafuu
MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:-
Licha ya Serikali kupeleka umeme vijijini kwa kasi kupitia mradi wa REA, bado kuna changamoto za kuunganisha umeme kwa wananchi.
(a) Je, Serikali ina mpango gani kuwawezesha wananchi kupata umeme kwa bei nafuu?
(b) Nguzo za umeme zinasimikwa kwenye njia kuu tu; je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha nguzo hizi zinapelekwa kwenye vitongoji?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Godfrey William Mgimwa, Mbunge wa Kalenga, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuwezesha wananchi kupata umeme kwa gharama nafuu, Serikali kupitia mradi kabambe wa kusambaza umeme vijijini (REA) inaunganisha umeme kwa gharama ya shilingi 27,000 tu na hii ikiwa ni Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) imepunguza gharama za umeme kwa kuondoa gharama za malipo ya maombi ya kufungiwa umeme yaani shilingi 5,000 pamoja na malipo ya huduma ya kila mwezi (service charge) ambayo ni shilingi 5,520 kwa wateja wote wa majumbani; hatua hii imeanza tangu tarehe 1 Aprili, 2016.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuwekeza zaidi katika uzalishaji wa umeme kwa kutumia vyanzo vya gesi asilia, joto-ardhi, jua, maji na makaa ya mawe pamoja na tungamotaka, ili kupunguza gharama za umeme zaidi.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, nguzo nyingi zimesimikwa kwenye njia kuu, hata hivyo katika Mpango wa REA Awamu ya Tatu utakaoanza bada ya bajeti yetu kupita mwezi Julai mwaka huu, maeneo mengi ya vitongoji yatafikiwa kwa kupewa huduma ya umeme, ili kurahisisha shughuli za uchumi za wananchi wa maeneo ya Kalenga.