Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 4 Good Governance Ofisi ya Rais TAMISEMI. 41 2016-01-29

Name

Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. KASUKU S. BILAGO aliuliza:-
Kifungu cha 3 cha Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003, na Kifungu cha 1(26) cha Kanuni za Kudumu za mwaka 2009 vinatoa tafsiri ya neno mwajiri kuwa ni mtu au taasisi ambayo mtumishi wa umma anaingia naye mkataba wa ajira na kumlipa mshahara.
Je, kwa kuzingatia tafsiri hiyo, mwalimu ambaye ni mtumishi wa umma, mwajiri wake ni nani?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (UTUMISHI NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchukua fursa hii kujibu swali la Mheshimiwa Mwalimu Kasuku Samson Bilago Mbunge wa Jimbo la Buyungu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mwajiri wa watumishi wote wa umma wakiwemo walimu ni Serikali ambayo ndiyo inakusanya mapato na kulipa mishahara ya watumishi wake. Hata hivyo, Serikali imekasimu madaraka kwa mamlaka mbali mbali kama ilivyoainishwa kwenye kifungu cha 6(1) cha sheria ya Utumishi wa Umma Sura ya 298.
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya kutungwa kwa sheria ya Tume ya Utumishi wa Walimu, sheria namba 25 ya mwaka 2015, Idara ya Utumishi wa Walimu ndiyo ilikuwa Mamlaka ya Ajira na nidhamu kwa walimu wote walio kwenye Utumishi wa Umma. Baada ya kutungwa kwa sheria hiyo ya Tume ya Utumishi wa Walimu namba 25 ya mwaka 2015, iliyoanzisha Tume ya Utumishi wa Walimu.
Tume hii sasa ya Watumishi wa Walimu pamoja na majukumu mengine itakuwa Mamlaka ya Ajira na Nidhamu kwa Walimu wa shule za msingi na sekondari walioajiriwa na Serikali.
WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS (UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika samahani.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutekeleza jukumu la kuwa mwajiri, Serikali huingia Mikataba ya Ajira na kulipa mishahara ya Walimu kupitia mamlaka za Serikali za Mitaa wanakofanyia kazi.