Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 21 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 180 2016-05-17

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:-
Wilaya ya Liwale ilipandishwa hadhi kuwa Wilaya kamili tangu mwaka 1975, lakini ni Wilaya ya pekee ambayo haina Kituo cha Polisi wala nyumba za watumishi wa kada hiyo:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga jengo la kituo cha Polisi Wilaya ya Liwale sambamba na nyumba za watumishi ambao wanaishi uraiani kwa sasa?
(b) Je, ni lini Tarafa ya Kibutuka itapata kituo kidogo cha Polisi ili kulinda wafanyabiashara wa mazao ya ufuta wanaokuja Tarafani?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamedi Kuchauka, Mbunge wa Liwale, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, siyo kweli kwamba Wilaya ya Liwale ndiyo Wilaya pekee nchini ambayo haina Kituo cha Polisi na nyumba za watumishi. Liwale ni miongoni mwa Wilaya 65 nchini ambazo bado hazijajengewa vituo vya Polisi.
Hata hivyo, Serikali itajitahidi kujenga vituo vya Polisi awamu kwa awamu kadri hali ya kibajeti itakavyoruhusu.
(b) Mheshimiwa Spika, ili kusogeza huduma za Polisi kwa wananchi ni azma ya Serikali kujenga Kituo cha Polisi kila Tarafa, sanjari na kupeleka Wakaguzi wa Polisi kuongoza vituo hivi, hata hivyo, Kata nne ikiwemo Kibutuka, Mirui, Kiangala na Nangano za Tarafa ya Kibutuka, kuna Askari Kata ambao wanatoa huduma kwa wananchi. Aidha, katika kutekeleza azma hii tayari Jeshi la Polisi limeshapeleka Wakaguzi katika baadhi ya Tarafa. Tunaomba Mheshimiwa Mbunge kuwa na subira kwani hali ya fedha itakaporuhusu mpango huu utafika kila Tarafa ikiwemo Kibutuka.