Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 23 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 194 2016-05-19

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:-
Utekelezaji wa maagizo ya Serikali Kuu kwa Halmashauri imekuwa ni changamoto na mzigo mkubwa kwa Halmashauri hizo hususan Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambapo maagizo mengi hayamo kwenye Mpango wa Bajeti na hivyo utekelezaji unakuwa mgumu.
Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha maagizo hayo yanatengewa bajeti?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa kwa nyakati tofauti Serikali imekuwa ikitoa maagizo ya kiutendaji katika Halmashauri zetu nchini na si kwa Halmashauri ya Kibaha pekee ikiwa na lengo la kuhakikisha kuwa inatatua changamoto ambazo Halmashauri zinaikabili kwa kipindi hicho.
Mheshimiwa Spika, baadhi ya maagizo hayo ya hutolewa na Serikali huhitaji fedha. Maagizo hayo huingizwa kwenye mipango na bajeti ya Halmashauri yanapotolewa kabla ya bajeti kupitishwa, hata hivyo baadhi ya maagizo na maelekezo hutolewa na Serikali katikati ya mwaka wa bajeti, maagizo na maelekezo ya Serikali ambayo hukosa kabisa fedha katika mwaka husika huingizwa katika bajeti za Halmashauri ya mwaka wa fedha unaofuata kwa ajili ya utekelezaji au Halmashauri hufuata utaratibu wa kurekebisha bajeti.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuzihimiza Halmashauri zote nchini, ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kuendelea kutenga fedha katika mpango na bajeti yao ili ziweze kutatua changamoto zinazowakabili.