Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 24 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 201 2016-05-20

Name

Dua William Nkurua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. WILLIAM D. NKURUA) aliuliza:-
Wilaya ya Nanyumbu ilianzishwa mwaka 2005 lakini mpaka sasa haina Hospitali ya Wilaya hivyo kuwalazimu wananchi kufuata huduma hiyo katika Hospitali ya Wilaya ya Masasi lakini pia kumekuwa na jitihada za kuomba kukipandisha hadhi Kituo cha Mangaka kuwa Hospitali ya Wilaya ya Nanyumbu lakini mpaka sasa hakuna mafanikio yoyote.
Je, Serikali haioni umuhimu wa kukipandisha hadhi kituo hicho ili kuwa Hospitali ya Wilaya na kunusuru afya za wananchi wa Nanyumbu hasa akina mama wajawazito kwa kulazimika kupelekwa Wilaya jirani ya Masasi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa William Dua Nkurua, Mbunge wa Nanyumbu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha Wilaya ya Nanyumbu inakuwa na Hospitali ya Wilaya, tayari Serikali imetoa kibali na kupandisha hadhi Kituo cha Afya cha Mangaka kuwa Hospitali ya Wilaya baada ya kukidhi vigezo na taratibu zilizowekwa. Kibali hicho kimetolewa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia barua ya tarehe 27 Februari, 2016.