Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 67 2022-04-19

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Buza-Kilungule hadi Nzasa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Nassoro Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Buza-Kilungule hadi Nzasa ina urefu wenye jumla ya kilomita tisa. Barabara hii imekasimiwa kwenye mtandao wa barabara zinazohudumiwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia Wakala wa barabara TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo katika hatua za utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami kuanzia Nzasa hadi Buza kupitia Mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam yaani Dar es Salaam Metropolitan Development Project. Mradi huu wa DMDP unasimamiwa na Wizara ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI na kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini (TARURA). Aidha, kwa sasa mkandarasi yupo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami. Ahsante.