Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 6 2023-01-31

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: -

Je, nini mkakati wa Serikali kuondoa changamoto ya Lumbesa kwa wakulima wa zao la viazi nchini?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA aljibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Festo Richard Sanga, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali kupitia Sheria ya Vipimo, Sura 340, mapitio ya mwaka 2002 na marekebisho yake ya mwaka 2018 wa kuondoa changamoto ya lumbesa ni kuendelea kutoa elimu kwa umma juu ya matumizi sahihi ya vipimo. Mazao ya mashambani ikiwemo viazi yatafungashwa kwa uzito usiozidi kilogramu 100 na hatua zitachukuliwa kwa wote watakaobainika kuvunja sheria hiyo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.