Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 57 2023-02-03

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG'WASI D. KAMANI aliuliza: -

Je, Serikali inatoa kauli gani kwa Makampuni Binafsi yanayouza Hisa na hayajatoa gawio miaka mingi pamoja na kujiendesha vizuri?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ng’wasi Damas Kamani, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ulipaji wa gawio kwa wanahisa wa kampuni unafanyika kwa kuzingatia Kifungu cha 180 cha Sheria ya Kampuni, Sura 212.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria hii, Serikali haiwezi kuingilia maamuzi na taratibu za kampuni kulipa gawio. Aidha, napenda kutoa rai kwa wanahisa wa kampuni mbalimbali kushiriki vikao vya mwaka vya wanahisa katika kampuni zao ili kuwa sehemu ya maamuzi yanayotolewa kwenye Mikutano Mikuu wa Mwaka.