Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 21 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 183 2022-05-12

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: -

Je, Serikali inaichukulia hatua gani TARURA Msalala kwa kuchelewesha mikataba na kuwapa kazi wakandarasi wasio na uwezo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Jimbo la Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/ 2022, jumla ya mikataba 11 inatekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala yenye jumla ya Shilingi bilioni 2.66. Kati ya Mikataba hiyo 11 Mikataba minane ilisainiwa mwezi Agosti, 2021 na Novemba, 2021 ambayo yote inatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Juni, 2022.

Mheshimiwa Spika, mikataba mitatu haikufikia hatua ya kusainiwa kutokana na kutopatikana kwa Makandarasi kwa wakati baada ya kushindwa kukidhi vigezo vilivyowekwa kwenye zabuni. Hivyo, Mikataba hiyo mitatu imesainiwa mwezi Februari na Machi, 2022 baada ya kuwapata Makandarasi waliopata zabuni.

Mheshimiwa Spika, kutokana maelezo hayo, Makandarasi wanaotekeleza mikataba minane imesainiwa kwa wakati kwa mujibu wa taratibu za ununuzi na mikataba mitatu ilichelewa kusainiwa kutokana na kushindwa kupatikana Makandarasi na zabuni kutangazwa upya.