Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 21 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 185 2022-05-12

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: -

Je, nini juhudi za Serikali kuweka mifumo rafiki ya kurahisisha ufanyaji wa biashara ili kuvutia zaidi uwekezaji nchini?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tarimba Gulam Abbas, Mbunge wa Kinondoni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kufanya maboresho ikiwa ni pamoja na kurekebisha sheria, kuweka mifumo ya kielektroniki, kufuta au kupunguza tozo na ada kero, kuondoa muingiliano wa majukumu katika baadhi ya taasisi, kuunganisha mifumo ya kielektroniki katika taasisi mbalimbali ili iweze kuwasiliana, kuweka miongozo na taratibu za utoaji huduma katika mamlaka za udhibiti, kuanzisha vituo vya pamoja vya kutoa huduma, kusogeza huduma karibu na watumiaji, kuboresha mifumo ya ukaguzi wa pamoja, kuweka utaratibu wa ukaguzi unaozingatia vihatarishi, kujenga uwezo katika mamlaka za uthibiti na kuweka taratibu na kanuni za kujidhibiti. Nakushukuru.