Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 21 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 186 2022-05-12

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI K.n.y. MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaongeza fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa REA III katika Wilaya za Busokelo na Rungwe?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nashukuru. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika utekelezaji wa Mradi wa REA awamu ya tatu (REA III) awamu ya kwanza jumla ya Vijiji 47 vimepatiwa umeme katika Halmashauri ya Busokelo, na Vijiji 22 katika Halmashauri ya Rungwe. Aidha, katika utekelezaji wa Mradi wa REA III round two, Vijiji vyote 32 vilivyobaki bila umeme katika Halmashauri ya Rungwe na Kijiji kimoja kilichobaki bila umeme katika Halmashauri ya Busokelo vitapatiwa umeme.

Mheshimiwa Spika, Mkandarasi M/S Electrical Transmission and Distribution Construction and Maintenance Co. LTD aliyepewa kazi ya kutekeleza mradi katika Mkoa wa Mbeya anaendelea na kazi katika maeneo ya Vijiji vya Busokelo na Rungwe ambapo wateja wa awali 594 wataunganishwa kwa huduma ya umeme.

Mheshimiwa Spika, gharama ya mradi ni Shilingi Bilioni 5.133. Serikali itaendelea kuongeza fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kufikisha umeme katika maeneo yote ya vitongoji vya Halmashauri za Busokelo na Rungwe kulingana na upatikanaji wa fedha.