Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 31 2023-04-06

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaangalia upya mipaka ya kiutawala ikiwemo na Halmashauri ya Mji wa Makambako?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikizingatia suala la maendeleo ya mipaka ya maeneo ya utawala ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi na kusogeza huduma karibu na wananchi.

Mheshimiwa Spika, mabadiliko ya mipaka ya maeneo ya utawala kwa mujibu wa mwongozo wa uanzishaji wa maeneo ya utawala katika mamlaka za Serikali za Mitaa wa mwaka 2014 huanza na kusudio ambalo hupaswa kujadiliwa katika vikao vya Ngazi ya Halmashauri, Wilaya na Mkoa. Kusudio hilo huwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kupitia Katibu Tawala wa Mkoa.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI bado haijapokea kusudio la kubadili mipaka kutoka Halmashauri ya Mji wa Makambako. Hivyo, endapo kuna uhitaji wa kubadili mipaka, inashauriwa kuanzisha kusudio na kuliwasilisha katika vikao vya Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango, Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) na hatimaye katika Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC).