Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 3 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 32 2023-04-06

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawaajiri Wataalam wanaojitolea kwa muda mrefu kufanya kazi katika Hospitali mbalimbali nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felista Deogratius Njau, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwenye hospitali zetu kumekuwa na watumishi wanaojitolea. Wizara imetoa Mwongozo wa kuwalipa nusu mshahara kwa mapato ya ndani. Hata hivyo hospitali zetu za Mikoa, Kanda na Taifa zimeweza kuwalipa hadi asilimia 40 ya watumishi wote wanaojitolea mshahara kamili kwa kutumia mapato ya ndani.

Mheshimiwa Spika, Wizara itashirikiana na Wizara ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kuona namna bora ya kuwapa kipaumbele kwenye ajira watumishi ambao wamekuwa wakijitolea kwenye vituo vya huduma za Afya kuliko walioko nje wakisubiri ajira.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.