Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 3 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 34 2023-04-06

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi katika Ziwa Victoria na Tanganyika?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kavejuru Eliadory Felix, Mbunge wa Jimbo la Buhigwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ina Mkakati wa Kuendeleza Sekta ya Uvuvi 2022/2023 – 2025/2026, pia Mkakati wa Taifa wa Kuendeleza Ukuzaji Viumbe kwenye Maji 2018 – 2025, na Mpango Kabambe wa Sekta ya Uvuvi 2021/2022 –2036/2037 ambayo imelenga kuongeza viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi kupitia Mkakati Jumuishi wa Kuendeleza Viwanda Nchini.

Mheshimiwa Spika, kupitia mikakati hiyo, Serikali imeendelea kuboresha miundombinu ya uvuvi na viwanda na uboreshaji wa mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji ambayo utekelezaji wake utaendelea kuvutia uwekezaji wa viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi nchini ikiwa ni pamoja na eneo la Ziwa Victoria na Tanganyika.