Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 47 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 402 2016-06-21

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:-
(a) Je, Serikali itakubali kujenga Hospitali ya Wilaya ya Busokelo hasa ikizingatiwa kuwa wananchi wametoa eneo tayari na wako tayari kushirikiana na Serikali?
(b) Je, kama Serikali inakubali, ni lini kazi hiyo itaanza?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Fredy Atupele Mwakibete, Mbunge wa Busokelo lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni sera ya Serikali kuhakikisha tunajenga hospitali kila Wilaya, ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi. Utekelezaji umefanyika kupitia mpango wa Halmashauri kwa kushirikisha nguvu za wananchi, hivyo napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha Hospitali ya Wilaya inajengwa katika Halmashauri mpya ya Busokelo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa hospitali hiyo umepangwa kuanza katika mwaka wa fedha 2016/2017 ambapo zimetengwa shilingi bilioni 2.0 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD).