Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 68 2023-04-13

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga majengo katika Kituo cha Afya Nguruka kilichopandishwa hadhi ya kuwa Hospitali?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Nguruka kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma kinahudumia wakazi wapatao 135,546. Kituo kinatoa huduma kwa ngazi ya kituo cha afya kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza imekwisha jenga hospitali mpya ambayo imeanza kutoa huduma.

Mheshimiwa Spika, kituo hiki kina uhitaji wa majengo mbalimbali ya kutolea huduma ikiwa ni pamoja na wodi mbili za kulaza wagonjwa, kliniki ya mama na mtoto, jengo la kuhifadhia maiti na jengo la kufulia.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 kituo hicho kimetengewa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu hiyo itakayowezesha kutoa huduma kwa ngazi ya kituo cha afya. Ahsante.