Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 69 2023-04-13

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya mchepuko kwa kiwango cha lami kutoka Mpemba kupitia Chapwa Mwakakati katika Mji wa Tunduma kwa kiwango cha lami?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwa sasa Mji wa Tunduma umekuwa ukikumbwa na msongamano mkubwa wa magari kuanzia Mpemba hadi Forodhani (Boarder) hali inayosababisha usumbufu kwa watumiaji wa barabara ya ndani ya Tunduma na wanaokwenda uelekeo wa barabara ya Tunduma - Sumbawanga.

Mheshimiwa Spika, ili kupunguza adha hiyo, Serikali itatenga kiasi cha shilingi bilioni 1.5 katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Sogea - Transformer yenye urefu wa kilometa 2.0 kwa kiwango cha lami ili iwe njia mbadala kwa watumiaji wa barabara za Mji wa Tunduma.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya barabara ya mchepuko inayoanzia Mpemba – Chapwa - Makambini kadri ya upatikanaji wa fedha ili kuondoa msongamano mkubwa wa magari. Ahsante.