Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 71 2023-04-13

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha utekelezaji wa Sera ya kupeleka umeme Vijijini kupitia Mpango wa REA III Mzunguko wa Pili?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mohamed Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi wa kusambaza umeme vijijini, awamu ya tatu mzunguko wa pili unaosambaza umeme vijijini vikiwemo vijiji vya Kilwa Kusini vyote, unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba, 2023. Aidha, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan imeongeza wigo wa mradi toka kilomita moja kwa kila kijiji na kufikia kilomita tatu (1+2) katika usambazaji wa umeme katika vijiji ili kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Mheshimiwa Spika, awamu hii ya REA III Round II itakapokamilika hakuna kijiji ambacho kitabaki bila umeme.