Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 6 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 72 2023-04-13

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: -

Je, lini Serikali itapitia upya masharti ya fomu za bima ya afya ili kuondoa upotevu wa fedha za Vituo vya Afya kwa kushindwa kujaza fomu hizo?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Jonathan Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini na Balozi wa Afya ya Akili kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, makato ya madai ya bima ya afya kwa watoa huduma za afya hayasababishwi na vipengele vilivyoainishwa katika fomu za bima ya afya (Fomu 2A na B). Sababu za Makato ya madai husababishwa na: -

(i) Kutozingatiwa kwa miongozo ya Tiba nchini inayotolewa na Wizara ya Afya;

(ii) Baadhi ya watoa huduma kuwasilisha madai yenye udanganyifu katika utoaji wa huduma;

(iii) Kutozingatiwa kwa bei zinazoainishwa katika Mkataba wa Huduma baina ya Mfuko na Watoa Huduma; na

(iv) Kutozingatiwa kwa taratibu za uwasilishaji wa madai ulioainishwa na Mfuko kwa mujibu wa Mkataba.