Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 73 2023-04-13

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuruhusu Mabasi ya Abiria yanayopita Wilayani Sikonge kuendelea na safari badala ya kuyalazimisha kulala?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI, alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Taska Mbogo Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua mabasi ya abiria yanayokwenda Mpanda Mkoa wa Katavi ambayo yanapita Wilaya ya Sikonge zaidi ya saa nne usiku hushauriwa kulala Sikonge kwa sabubu za kiusalama. Eneo hilo lina pori la hifadhi kuanzia Sikonge hadi Inyonga lenye urefu wa kilometa 161 na halina mtandao wa mawasiliano. Hivyo si salama kupita nyakati za usiku mkubwa.

Mheshimiwa Spika, ili kuepuka adha ya kutakiwa kulala Sikonge, wamililki wa mabasi ya abiria wanashauriwa kupanga safari zao ili wapite katika maeneo hayo yenye changamoto mapema zaidi. Mabasi hayo yanaweza kuomba kuanza safari zao hasa kutoka Dar es Salaam saa tisa au saa kumi Alfajiri na Serikali itaafiki maombi yao.