Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 6 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 75 2023-04-13

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: -

Je, ni upi mkakati wa kurahisisha matumizi ya Kibenki kwa njia ya Simu kwa kutumia bando za simu badala ya salio la simu la kawaida?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Judith Salvio Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kurahisisha matumizi ya Kibenki kwa njia ya Simu kwa kutumia Bando za Simu badala ya salio la Simu la kawaida, utaratibu umewekwa kwamba unapokuwa na kifurushi cha data unaweza kutumia huduma za kibenki zinazotumia programu tumizi kama SIM Banking App na nyinginezo ili kuweza kupata huduma za kibenki.

Mheshimiwa Spika, pale ambapo mtumiaji anatumia namba fupi fupi (USSD) ambazo ni huduma za ziada, mtumiaji anaweza kulipishwa ama kutolipishwa gharama za ziada; suala hili linategemea makubaliano kati ya benki na watoa huduma za mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, ili kuongeza wigo wa matumizi ya fedha, Msimamizi wa huduma za kifedha anaweza kuwaelekeza watoa huduma za kifedha kuingia mikataba na watoa huduma za mawasiliano, badala ya kuwalipisha wanaotumia namba fupifupi kwenye huduma za kifedha.