Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 6 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 78 2023-04-13

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kupanda Hifadhini mazao yanayofuatwa na wanyama waharibifu kutoka Hifadhi za Rungwa, Muhesi na Kizigo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na changamoto ya ongezeko la matukio ya wanyamapori kuingia kwenye makazi ya watu na kusababisha madhara kwa wananchi na mali zao. Changamoto hiyo imesababishwa na uanzishwaji wa shughuli za binadamu kwenye shoroba, maeneo ya mtawanyiko wa wanyamapori na maeneo ya pembezoni mwa hifadhi. Maeneo hayo hutumiwa na wanyamapori wanaohama kutoka katika mfumo mmoja wa ikolojia kwenda mfumo mwingine kwa ajili ya kutafuta maeneo ya malisho, maji, mazalia, ulinzi na mapumziko kwa nyakati tofauti.

Mheshimiwa Spika, kutokana na sababu hiyo ya kiikolojia, upandaji wa mazao katika hifadhi za wanyamapori hauwezi kuzuia wanyamapori kuhama kutoka mfumo mmoja wa ikolojia kwenda mfumo mwingine.

Vilevile upandaji wa mazao hifadhini ni ukiukwaji wa sheria za uhifadhi kwa kuwa wanyamapori wanaishi katika mazingira asilia ambapo mimea mingine ambayo siyo ya asili hairuhusiwi ndani ya hifadhi.