Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 79 2023-04-13

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Bwawa la Mandela Kwenjugo na Kamkole Mabanda?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Reuben Nhamanilo Kwagilwa Mbunge wa Handeni Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kuboresha huduma ya maji Wilayani Handeni, Serikali ipo kwenye hatua za mwisho za usanifu wa Mabwawa ya Mandela – Kwenjugo na Kamkole – Mabanda na usanifu huo utakamilika mwezi Juni, 2023. Ujenzi utaanza katika mwaka wa fedha 2023/2024. Kukamilika kwa ujenzi wa mabwawa hayo kutanufaisha wananchi wapatao 11,004 wa mitaa ya Mabanda, Komoza, Kwenjugo, Ngugwini, Bwila, Kwedisewa na Kwedigongo.