Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 7 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 83 2023-04-14

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: -

Je, ni lini Wananchi wa Sikonge watapatiwa eneo la hekta 33,000 kwenye Mbuga ya Ipembampazi litumike kwa kilimo na ufugaji?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Hifadhi ya Msitu wa Ipembampazi ina umuhimu katika kuimarisha mfumo wa ikolojia wa Ugalla - Moyowosi unaojumuisha maeneo ya hifadhi yaliyopo katika Mikoa ya Tabora na Kigoma ambapo eneo la msitu huo linatumika kama mtawanyiko na mapito ya wanyamapori hususan tembo. Eneo hilo lina wanyamapori wa aina mbalimbali na limetengwa kuwa kitalu cha uwindaji wa wenyeji.